Gazeti la kila siku El Confidencial leo limeripoti taarifa za ndani za mkataba unaosubiriwa kusainiwa baina ya Jose Mourinho na waajiri wake wapya Manchester United.
Taarifa za ‘Special One’ kubeba mikoba ya Van Gaal zimechapishwa na kila chombo cha habari huko England asubuhi ya leo.
Vichwa vya habari vya magazeti vimeandika kwamba: Jose Mourinho amewaambia marafiki wa karibu kwamba atakuwa boss mpya wa United kuanzia msimu ujao.
Taarifa zaidi kutoka kwenye sehemu ya mkataba wa Mourinho na United ni kwamba mkataba utakuwa wa kuanzia msimu wa 2016/17 mpaka 2019/20, huku akiweka kibindoni kiasi cha 20 million euros kwa mwaka.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni