TANGAZO

TANGAZO

Jumatano, 3 Agosti 2016

Tazama video maonesho ya nane nane mkoani ,morogoro yakiendelea huku Wananchi wa Tanzania waombwa kutumia hasa bidhaa zinazo tengeneza hapa nchini.



Wafanyabiashara na wakulima nchini wametakiwa kupenda bidha zinazozalishwa ndani ya nchi badala yake wasipendelee kutumia bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa mauzo kutoka Kampuni ya Old Ease International JOHN MCHARO mapema hii leo wakati akiongea na WIKESI BLOGS kwenye Maonesho ya Nane nane katika uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere mkoani Morogoro.

Kampuni hiyo inayohusika na kuzalisha vifaa mbalimbali vya Mashine za printer ndiyo ya kwanza hapa nchini Tanzania kuwa na kiwanda kinachozalisha bidhaa hiyo  Afrika Mashariki na Kati kwa ujumla.
Hata hivyo Mcharo amesema kuwa Maonesho ya Nane nane  yanayonedelea katika  viwanja hivyo vya Mwalimu Nyerere Mkoani Morogoro, yanafaa kutokana na wakulima wanapata elimu mbalimbali ikiwemo mbinu za kilimo cha kisasa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni