TANGAZO

TANGAZO

Jumatatu, 6 Julai 2015

Ally Kiba alivyopanda daladala kukutana na mashabiki Dar es salaam, akaulizwa kuhusu Diamond

Tazama video  ya alikiba akijibu maswali ya abilia kwenye daladala kutazama bofya

Video ikionyesha walichokifanya Abdu Kiba na Ruby nyuma ya Camera!

Abdu 1Ni dakika chache ambazo zinakutangulizia kuona kitachofata kwenye video mpya ya Abdu Kiba ft. Ruby (Ayaya) ambayo ni single mpya kwenye radio kwa wiki kadhaa sasa hivi.
Location ya hii video ni White Sand Dar es salaam Tanzania.

KUTAZAMA VIDEO HII BOFYA

KESHI ATUPIWA VIRAGO NIGERIA

KeshiShirikisho la Soka nchini Nigeria limetangaza kumsitishia ajira ya kuinoa timu ya Taifa ya Nigeria ‘The Super Eagles’ kocha Steven Keshi.

Siku saba za urais ndani ya CCM


Dar/Dodoma. Ni wiki ngumu kwa Chama cha Mapinduzi (CCM). Ndivyo unavyoweza kusema kwani chama hicho kinachotawala kitafanya vikao vyake vya juu vitakavyohitimishwa kwa kumpata mgombea wake wa urais.

Kikwete: Msimchague huyu




Tanga. Rais Jakaya Kikwete amewataka viongozi wa dini nchini kuwahimiza waumini wao kuwachagua wanasiasa wasiokuwa waovu, wasiofanana na uovu au hata kuukaribia.
Amewataka kuepuka makundi ya kisiasa na wasiwape mwanya wanasiasa wenye dhamira ovu katika kutafuta madaraka kwa thamani yoyote na wawakemee wale wanaotaka kupata madaraka kwa gharama yoyote.

Mbunge ajivua uanachama Chadema


Sumbawanga. Mbunge wa Mpanda Mjini, Said Arfi ametangaza kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Akizungumza mjini Mpanda katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kashaulili, jana Arfi aliwaeleza wananchi wa Mpanda kuwa uanachama wake ndani ya Chadema utakoma mara tu baada ya kuvunjwa Bunge Julai 9.

Ijumaa, 3 Julai 2015

Upinzani ‘walianzisha’ tena bungeni




Dodoma. Mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika jana ulizua kizaazaa na kumlazimisha Spika Anne Makinda kuahirisha kikao baada ya kukosekana utulivu ndani ya Ukumbi wa Bunge.
Kikao hicho kiliahirishwa muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu wakati Bunge lilipotakiwa kukaa kama kamati kumalizia kiporo cha Muswada wa Sheria ya Kuwalinda Watoa Taarifa za Uhalifu na Mashahidi wa mwaka 2015 ambao mchakato wa kuupitisha haukukamilika juzi kutokana na muda kuisha.

Alhamisi, 2 Julai 2015

Rick Ross ni jela au mtaani? Haya hapa kutoka Mahakamani na video yake..

       Rick-Ross-court


Headlines za Entertainment Marekani zilikuwa na story ya Rick Ross kukamatwa na kuwekwa ndani yeye pamoja na bodyguard wake, kesi yao ilikuwa ni ishu ya kuteka na kujeruhi watu wawili.
July 01 2015 kapandishwa Mahakamani, Georgia Marekani.. Kesi ikasomwa na milango ikawa wazi kwa jamaa kuwekewa dhamana

Watuhumiwa wa EPA Waachiwa Huru.

  

 MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewaachia huru Kada wa CCM Rajabu Maranda na wenzake waliokuwa wanakabiliwa na kesi wizi wa Sh milioni 207 katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

 
Jopo la mahakimu watatu likiongozwa na Hakimu John Utamwa, Ignas Kitusi na Eva Nkya liliwaachia washitakiwa hao baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi ya washitakiwa hao.

Chadema yaibwaga ccm Mahakamani

Kiteto. Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara imezidi kupata pigo baada ya Mahakama kutengua matokeo ya uchaguzi wa wenyeviti wa vitongoji 16 vya mji mdogo wa Mirerani, kwa maelezo kuwa ulikiuka sheria na utaratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Hii ni mara ya pili katika kipindi cha mwezi mmoja kwa Mahakama kutengua matokeo ya uchaguzi huo ambao uliwaweka madarakani makada wa CCM.

LOWASA ACHOKA KUITWA FISADI

     


Dodoma. Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa jana aliwataka wanaomhusisha na ufisadi kuacha mara moja kwa sababu hakuna hata chembe ya ukweli katika tuhuma hizo.
Lowassa, aliyeonekana kuzungumza kwa hisia, alisema hayo jana mara baada ya kurejesha fomu ya kuwania kuteuliwa na CCM kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.

ALIKIBA ATOA MAJIBU JUU YA KUTO FOLLOW MTU

             alikiba

 Je Ushawai Kujiuliza Hivi Mbona Msanii wa Bongo Flava ALIKIBA ( @officialalikiba ) Ha Follow Mtu Yeyote Kwenye Mtandao Wa Instagram?? >>>>>>> Hivi Majuzi Tulikutana na Mwimbaji huyo wa MWANA na Tukamuuliza hivi Mbona ha follow mtu kwenye mtandao wa Insta, na Hii ndio ilikuwa jibu lake ” Yea si follow mtu kwasababu, kwanza kabisa nafanya kazi na watu wengi kuna akina TUVA kuna watu kibao lakini watu wa Media ndio tuko nao karibu,sasa wengine walikua waki complain nikawa naogopa zile lawama nilichoshauriwa na hao wenyewe kwamba ni heri ni si follow mtu na vile vile nilipenda ivyo kutokana na promotion ya ujio wangu ambao ulikuwa unakuja ili niweze ku concetrate na account yangu nijue mafans wangu wanataka kitu gani wanani advice kitu gani na pia imesaidia naona jinsi gani wako serious namimi kwasababu naongea nao,kuna wengine wananipa challenge kuna matusi uhmm ni vitu vya kawaida na vile vile wanapokuwa wananisema wananijenga wananitengeneza kiasi fulani,wananibadilisha ni wapi nimekosea naweza kubadilisha” Alisema ALIKIBA ambaye hivi majuzi ameachia Video ya Wimbo Wake ‘Chekecha’. Interview nzima unaweza kuisikiliza ndani ya #MamboMseto ya Radio Citizen. By @sameerbry1

Jumatano, 1 Julai 2015

WALIOMUUA ALBINO MWAKAJILA WA MBEYA WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI

Hakimu Mwakalinga siku alipohukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa mauaji ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe. Leo amehukumiwa tena kunyongwa mpaka kufa katika mauaji ya mlemavu wa ngozi Henry Mwakajila.
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Mbeya leo hii imewahukumu kunyongwa mpaka kufa watu wanne kati ya watano waliomuua Henry Mwakajila (17) ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino).
Waliohukumiwa kunyongwa mpaka kufa ni Asangalwisye Kayuni maarufu kama Katiti au Mwakatoga na Gerard Korosso Kalonge (wakazi wa Kijiji cha Mbembati wilayani Ileje), na Leonard Msalage Mwakisole na Hakimu Mselem Mwakalinga (wakazi wa Kiwira wilayani Rungwe).
Mshtakiwa wa nne, Mawazo Philemon Figomole, ameachiliwa huru na mahakama hiyo baada ya ushahidi wa upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha pasi na shaka kwamba alihusika katika mauaji hayo.

Lowassa arejesha fomu za Uraisi, atoa onyo kali

 
         
 
Baada ya kukabidhi fomu hizo, Mh. Lowassa, alikutana na waandishi wa habari na kusoma taarifa yake fupi, ambapo alionya wale wote wanaoeneza habari potofu kuwa yeye ni mla rusha, watoe ushahidi, wapi amekula rushwa, na ni  kiasi gani, za nani na wapi, Awataka Watanzania kupuuza habari hizo na kwani yeye ni muadilifu na hana shaka na hilo.

MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA TANO 2015 YATANGAZWA

Jumla ya wanafunzi 18,751 kati ya 73,754 (asilimia 74.58) waliofanya mitihani ya kidato cha nne mwaka jana wamekosa nafasi za masomo za kujiunga kidato cha tano na vyuo vya ufundi mwaka huu kutokana na sababu mbalimbali.
Miongoni wa sababu hizo ni ufinyu wa nafasi za shule, kushindwa kupata ufaulu wa masomo waliyochagua, umri mkubwa wa watahiniwa wa kujitegemea pamoja na kukosa sifa za kuchaguliwa, huku muhula wa kwanza wa kujiunga kidato cha tano ukitarajiwa kuanza Julai 18, mwaka huu.
Aidha, wanafunzi 479 wakiwamo wavulana 332 na wasichana 147 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya ufundi mwaka huu, huku idadi ya wanafunzi hao ikiongezeka kutoka 472 mwaka 2014 hadi 479 mwaka huu.