TANGAZO

TANGAZO

Jumatatu, 6 Julai 2015

KESHI ATUPIWA VIRAGO NIGERIA

KeshiShirikisho la Soka nchini Nigeria limetangaza kumsitishia ajira ya kuinoa timu ya Taifa ya Nigeria ‘The Super Eagles’ kocha Steven Keshi.

Keshi,53, ambaye aliteuliwa tena kukinoa kikosi hicho mwezi April mwaka huu, ametimuliwa jana jioni, huku msaidizi wake Salisu Yusuf pamoja na Kurugenzi ya Ufundi ya Shirikisho hilo chini Amodu Shuaibu, wakishika nafasi hiyo mpaka maamuzi mengine yatakapotangazwa.
“Baada ya kuipitia mara kadhaa ripoti ya Kamati ya Nidhamu na kamati ya Ufundi na Maendeleo ya NFF, lakini vilevile mwenendo na matendo ya Keshi kama kocha mkuu, tumegundua kuwa kuna ukosefu wa dhamira ya dhati wa kufikia malengo ya Shirikisho kama ilivyoainishwa katika makubaliano ndani ya mkataba,” ilisomeka taarifa iliyotolewa na kamati ya utendaji ya NFF.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni