rooney
Wayne Rooney.
henry
Thierry Henry.
Na Mwandishi wetu,
Nahodha wa Manchester United, Wayne Rooney amefanikiwa kuvunja rekodi iliyokuwa imewekwa na mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry baada ya kuifungia klabu yake katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Liverpool.
Rooney amevunja rekodi ya Henry ya kufunga magoli mengi kwenye michezo ya ligi kuu wa Uingereza kwa kuchezea timu moja ambapo Henry alikuwa na rekodi ya kufunga magoli 175 katika michezo 258 na aliyafunga kwa kipindi cha mwaka 1999-2007 na baadae kwa mkopo kwenye msimu wa 2011-2012.