TANGAZO

TANGAZO

Jumanne, 5 Januari 2016

WAZIRI wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera,Uratibu na Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu,Mheshimiwa Jenista Mhagama afanya ziara ya ghafra Manispaa ya Morogoro



 PICHA:NA MAKTABA

NA THOMAS WIKESI
WAZIRI wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera,Uratibu na Bunge; Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu,Mheshimiwa Jenista Mhagama amewataka watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuacha kufanya kazi kwa mazoea endapo wanahitaji kuendelea kuwepo kazini.


Mheshimiwa Mhagama ametoa kauli hiyo hii leo mjini Morogoro katika aliyoifanya ya kukagua shughuli mbalimbali zinazofanywa na vijana ambapo ametoa muda wa siku saba kwa uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuwatafutia vijana maeneo maalumu ya kufanyia shughuli za kuzalisha mali.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Morogoro,Pasco Kihanga licha ya kukiri kuwepo kwa mapungufu katika utendaji kazi kwa baadhi yaa watumishi wa Manispaa hiyo ameiombaa Serikali kuhakikisha inawapatia vijana elimu ya biashara kabla ya kuwapatia fedha za mikopo kwa ajili ya kujiendeleza kiuchumi tofauti na ilivyo sasa.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni