TANGAZO

TANGAZO

Jumatatu, 4 Januari 2016

MTU MMOJA ADAIWA KUKUTWA AMEFARIKI LEO ASUBUHI JIJINI MBEYA.

Mtu mmoja Jijini Mbeya (PICHANI JUU) ambaye hakuweza kutambulika kwa Majina,inadaiwa amekutwa amefariki  leo asubuhi kwenye moja ya uchochoro  wa nyumba zilizopo katika mtaa wa Mwamfupe.

Kifo cha Mtu huyo ambaye inaelezwa ni kijana wa makamo alikutwa amefariki kwenye uchochoro wa nymba hiyo mara baada ya kubainika na baadhi ya Wananchi,waliokuwa wakikatiza mtaa huo kuelekea mtaa mwingine,Baadhi ya Mashudhua wa eneo hilo wameeleza kuwa mtu huyo si mkazi wa mtaa huo,

 "Mtu huyo si Mkazi wa Eneo hili, bali Jioni ya jana waliomuona maeneno hayo akiwa katika hali ya kupepesuka Pepesuka kotokana na kunywa Pombe, na huenda hicho ndicho kilicho pelekea Kifo chake kwani hakuwa mwenye afya njema." Alibainisha mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo wakati akihojiwa na Mwandishi wa Globu ya Jamii iliofika eneo la tukio
Baadhi ya Wanachi wa Mtaa wa Mwamfupe wakijadiliana jambo katika eneo la  tukio.
Huzuni  ikatawa Eneo hilo.
Baadhi ya Wanachi sambamba na Wenyenyumba zilizo zunguka Eneo hilo la Tukio wakisubiri msaada kutoka Jeshi la Polisi.Globu ya Jamii inafuatilia taarifa kamili kutoka kwa jeshi la Polisi mkoani Mbeya.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni