TANGAZO

TANGAZO

Alhamisi, 18 Februari 2016

Sentensi sita za NECTA kuhusu matokeo ya mitihani ya kidato cha nne 2015 .


February 18 baraza la mitihani Tanzania NECTA wametangaza matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2015 yafuatayo ni maneno matatu waliyosemwa na katibu mtendaji wa baraza la mitihani Tanzania NECTA Dk Charles Msonde.
“Katika mkutano maalum wa baraza wa 110 uliofanyika February 17 2016, baraza la mitihani Tanzania lilipitia taarifa ya matokeo ya kidato cha nne na maarifa uliofanyika tarehe 2 hadi 27 November 2015 na kuidhinisha kutangaza rasmi kwa matokeo hayo katika mitihani ya kidato cha nne 2015”

“Jumla ya watahiniwa 448382 waliandikishwa kufanya mtihani huo, wasichana ni 229144 na wavulana 219238 kati ya hao watahiniwa waliosajiliwa, watahiniwa wa shule walikuwa 394o65, wakati watahiniwa wa kujitegemea walikuwa 54317”
“Watahiniwa wa shule asilimia 96.71 walifanya mitihani na watahiniwa 14749 ambao sawa na asilimia 3.29 hawakufanya mtihani, watahiniwa wa kujitegemea 49333 sawa na asilimia 90.82 lakini watahiniwa 4984 sawa na asilimia 9.18 hawakufanya mtihani”
“Watahiniwa wa mtihani wa maarifa 19547 waliosajiliwa, lakini watahiniwa kati ya wale waliosajili 16162 sawa na asilimia 82.68 walifanya mtihani, lakini watahiniwa 3385 kati ya hao hawakufanya mtihani”
“Kwa jumla ya watahiniwa 272947 sawa na asilimia 67.53 ya watahiniwa waliofanya mtihani wa kidato cha nne wamefaulu mtihani, wasichana waliofaulu ni 131913 sawa na asilimia 64.84, wakati wavulana waliofaulu ni 141034 sawa na asilimia 71.09”
“lakini mwaka jana watahiniwa waliofaulu walikuwa  196805 sawa na asilimia 68. 33 hivyo ufaulu ukilinganisha na matokeo ya mwaka jana, ufaulu umeshuka kwa asilimia 0.8 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2014”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni