TANGAZO

TANGAZO

Ijumaa, 5 Februari 2016

UNAJUA KINACHOMUWEKA BENCHI MAGURI? MWENYEKITI WA STAND ATUMBUA JIPU

Elius Maguri, Mshambuliaji wa Stand United anatesa baada ya kutemwa MsimbaziElius Maguri, amejikuta akichezea mkeka ndani ya kikosi cha Stand United licha ya kuwa kwenye kiwango bora kwa sasa
Mshambuliaji wa Stand United Elius Maguli siku za hivi karibuni amekuwa haonekani dimbani kutokana na kuchezea mkeka ndani ya kikosi cha Stand United chini ya kocha mfaransa Patrick Liewig.

Baada ya kuligundua hilo, mtandao huu uliamua kumtafuta mwenyekiti wa klabu hiyo Amani Vicent kumuuliza kama striker huyo ambaye alianza ligi kwa kasi huku akitupia kambani mfululizo anatatizo lolote linalosababisha asugue bechi.

“Elius Maguli hana tatizo na uongozi wa Stand Unitd na kutokupangwa kwake kunatokana na program ya mwalimu mwenyewe alivyojiwekea maana yeye ndiyo mkuu wa benchi la ufundi, ikumbukwe Maguli aliondoka kwenda kufanya majaribio huko Misri aliporudi alikuwa amechelewa kujiunga na timu na vilevile mwalimu anasema yeye hakuwa ameagwa”, amesema mwenyekiti wa Stand United.

“Lakini siyo kesi sana, kwasababu program za kupanga kikosi zinakuwa chini ya mwalimu, kwahiyo sababu inawezekana ikawa hiyo lakini mechi ya Mtibwa alicheza, mechi ya FA Cup na Mwadui aliingia akacheza  kwahiyo nadhani lipo kwenye mikono ya kocha kama alikuwa amekwazwa na hilo au la, lakini sisi kama uongozi tulikubali akafanye trial maana kule kwenye klabu ya Zamalekh kama angekuwa amefaulu basi ilikuwa ni moja ya maendeleo kwake na klabu ya Stand kwasababu wachezaji kama hawa wanacheza kwa ajili ya kutafuta maisha lakini pia kulisaidia taifa”.

“Kwahiyo nafikiri kulikuwa na mawasiliano madogo kati ya kocha na uongozi nafikiri hilo pia limekuwa sababu lakini sababu nyingine ni za kocha mwenyewe kwasababu anakikosi kipana anaweza kufanya anavyoweza yeye kama mkuu wa benchi la ufundi”.

Maguli alikuwa kwenye kiwango bora tangu alipojiunga na Stand United baada ya kupigwa chini na ‘wekundu wa Msimbazi’ Simba. Maguli aliongoza orodha ya wafungaji kwenye ligi ya VPL na kupelekea kuitwa kwenye kikosi cha Taifa Stars lakini siku za hivi karibuni amejikuta akichoma mahindi kwenye benchi licha ya kuwa na kiwango cha hatari lakini inaonekana hakuna maelewano kati ya Maguli na kocha wa timu hiyo Patrick Liewig
Chanzo:Shafii Dauda

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni