TANGAZO

TANGAZO

Alhamisi, 4 Februari 2016

VPL: SIMBA MWENDO MDUNDO, YANGA YACHECHEMEA, MATOKEO, MSIMAMO NA WAFUNGAJI YAPO HAPA

SIMBA SC imejiweka sawa kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuifunga Mgambo JKT mabao 5-1 jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
http://1.bp.blogspot.com/-mYophk0enlc/VjG3Q2q8iOI/AAAAAAAAq2I/2JFGgKDo1Kw/s640/VPL-logo.jpg
Ushindi huo unaifanya Simba SC ifikishe pointi 39 baada ya kucheza mechi 17, sasa ikiwa inazidiwa pointi moja tu na mabingwa watetezi, Yanga SC walio kileleni, wakifuatiwa na Azam FC yenye pointi 39 pia.
Mshambuliaji Mganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ aliifungia Simba SC bao la kwanza dakika ya tano akimalizia krosi ya mshambuliaji Ibrahim Hajib.
Kiiza akakosa penalti dakika ya 14 iliyookolewa na kipa Mudathir Khamis, kufuatia Henry Chacha kuunawa mpira kwenye boksi
Lakini Mwinyi Kazimoto akafunga bao la pili dakika ya 28 kwa shuti kali kutoka nje ya boksi baada ya kugongeana vizuri na Hajib.

Hajib akaenda kufunga mwenyewe bao la tatu dakika ya 42 baada ya kuwachambua mabeki watatu wa Mgambo na kipa wao Mudathir Khamis, kufuatia pasi ya Kazimoto.

Daniel Lyanga aliyetokea benchi kuchukua nafasi ya Hajib kipindi cha pili, aliifungia Simba SC bao la nne kwa shuti kali kutoka nje ya boksi baada ya pasi ya kiungo Said Ndemla.

Kiiza akahitimisha karamu ya mabao ya Simba SC kwa kufunga bao la tano dakika ya 82 akimalizia krosi ya Hassan Kessy, ambaye amecheza kwa kiwango cha juu leo.

Fuluzulu Maganga ‘akachafua gazeti’ kwa kuifungia Mgambo bao la kufutia machozi dakika ya 88 baada ya mabeki wa Simba SC kumuacha wakidhani ameotea.

Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Vincent Angban, Kessy Ramadhani, Abdi Banda, Juuko Murshid, Hassan Isihaka, Justice Majabvi, Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude, Hamisi Kiiza, Ibrahim Hajib/Danny Lyanga dk72 na Hija Ugando/Said Ndemla dk62. 

Mgambo JKT; Mudathir Khamis, Bakari Mtama/Bolly Shaibu dk44, Salim Mlima, Salim Kipaga, Ramadhani Malima/Mussa Ngunda dk44, Henry Chacha, Sunday Magoja, Mohammed Samatta, Fully Maganga, Ally Nassor na Aziz Gilla. 
Kule Mbeya
YANGA SC imezidi kupoteza matumaini ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya jioni ya leo kulazimishwa sare ya 2-2 na Prisons Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Matokeo hayo hayaiondoi kileleni Yanga SC ikifikisha pointi 40 baada ya kucheza mechi 17, mbele ya Azam FC na Simba SC wenye pointi 39 kila mmoja.
Lakini Azam FC wana viporo wawili, wakati Simba SC ndiyo wamecheza mechi 17 kama Yanga. 
Yanga SC walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 35 kupitia kwa mshambuliaji wake Mrundi, Amissi Tambwe aliyefunga kichwa akimalizia krosi ya kiungo Mnyarwanda, Haruna Niyonzima.
Prisons wakasawazisha bao hilo kupitia kwa Jeremiah Juma Mgunda aliyefunga kwa kichwa pia dakika ya 40 akimalizia krosi ya Mohammed Mkopi.
Mkopi akaifungia Prisons bao la pili dakika ya 62 kwa kichwa pia akimalizia mpira wa adhabu uliopigwa na kiungo wa zamani wa Yanga SC, Juma Seif ‘Kijiko’.
Mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu uliopita, Simon Msuva aliyetokea benchi kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Deus Kaseke aliisawazishia Yanga kwa penalti dakika ya 84 baada ya beki Meshak Suleiman kuunawa mpira kwenye boksi.
Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Deo Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Vincent Bossou, Mbuyu Twite, Said Juma ‘Makapu’/Salum Telela dk59, Deus Kaseke/Simon Msuva dk54, Haruna Niyonzima na Donald Ngoma, Amissi Tambwe na Issoufou Boubacar.
Prisons; Benno Kakolanya, Benjami Asukile, Laurian Mpalile, James Mwasota, Nurdin Chona, Jumanne Fadhil, Lambert Sadianka, Freddy Chudu/Juma Seif dk48, Mohammed Mkopi, Jeremiah Juma na Leonce Mutalemwa/Meshack Suleiman dk51. 
MATOKEO YOTE KWA UJUMLA
FT
T.PRISONS
2
 : 
2
YANGA
FT
SIMBA SC
5
 : 
1
MGAMBO JKT
FT
KAGERA SUGAR
2
 : 
1
MAJIMAJI

JKT RUVU
0
 : 
0
MBEYA CITY
FT
AFRICAN SPORT
1
 : 
0
MWADUI FC
FT
MTIBWA SUGAR
2
 : 
2
TOTO AFRICANS


Orodha ya Wafungaji Bora Ligi Kuu Msimu Huu

RnPlayer NameTimuGoal
1Amisi TambweYanga SC14
2Hamisi KiizaSimba SC14
3Jerema JumaT.Prisons10
4Donald NgomaYanga SC9
5Elias MaguliStand United9
6Ibrahim AjibuSimba SC7
7Kipre TchecheAzam FC7
8Shomari KapombeAzam FC7
9Atupele GreenNdanda FC6
10John BoccoAzam FC6
11Fully Zully MagangaMgambo JKT5
12Mohammed MkopiT.Prisons5
13Paul NongaMwadui FC5
14Thaban KamusokoYanga SC5
15Didier KavumbaguAzam FC4
16Edward ChristopherToto Africans4
17Jery TegeteMwadui FC4
18Miraji AthumanToto Africans4
19Omary MpondaNdanda FC4
20Saimon MsuvaYanga SC4


Msimamo wa Ligi Kuu Msimu Huu

RnTimuPWDLFAGdPts
1YANGA1712413892940
2SIMBA SC17123232102239
3Azam FC15123030102039
4MTIBWA SUGAR179532011932
5MWADUI FC178451915428
6STAND UNITED169161713428
7T. PRISONS168441817128
8TOTO AFRICANS174671521-618
9MGAMBO SHOOTING164571417-317
10KAGERA SUGAR174310920-1115
11MBEYA CITY163581321-814
12NDANDA FC162771418-413
13Coastal Union162771117-613
14JKT RUVU163491623-713
15MAJIMAJI FC1734101031-2113
16AFRICAN SPORT173311519-1412

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni