TANGAZO

TANGAZO

Jumatano, 3 Februari 2016

Baba yake Neymar kataja kuwa imemfikia ofa ya pound milioni 144.4 kwa ajili ya Neymar, The Sun wataja klabu inayomtaka


Mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil anayeichezea klabu ya FC Barcelona ya Hispania Neymar, bado yupo kwenye headlines kuhusiana na suala lake la usajili kutoka Santos kujiunga FC Barcelona mwaka 2013, kudaiwa kuwa na magumashi kiasi cha yeye kufikishwa mahakamani kutoa ushahidi.

Moja kati ya stori zilizotumika kupamba headlines za gazeti la The Sun, ni stori kuhusu Neymar kuhusishwa kujiunga na klabu ya Man United ya Uingereza ambayao imetaja kutenga dau la uhamisho wa kihistoria katika soka la pound milioni 144.4.
sun
Stori za Neymar kuhitajika kwa dau la pound milioni 144.4 inaripotiwa kutolewa na baba yake mzazi, ambaye anasema kuwa tayari amepokea ofa ya pound milioni 144.4 kutoka kwa moja ya vilabu vya Ulaya lakini sio hakutja jina la klabu na kuongezea kuwa sio Real Madrid klabu hiyo, uchunguzi wa The Sun unatajwa kufanikiwa  kujua jina la klabu ambayo inatajwa kuwa ni Man United.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni