TANGAZO

TANGAZO

Jumanne, 29 Desemba 2015

Kipindupindu chashika kasi Nyamagana, Magu

Mwanza. Ugonjwa wa kipindupindu umeendelea kuzitesa Wilaya za Nyamagana na Magu mkoani hapa, baada ya idadi ya wagonjwa kuongezeka na kufikia 17, huku mtu mmoja akipoteza maisha wilayani Magu.
Akizungumza na gazeti hili jana, Kaimu Mganga Mkuu wa mkoa, Dk Rwekyendela Onesmo alisema licha ya jitihada zinazofanywa, ugonjwa huo unazidi kuzikumba baadhi ya wilaya za mkoa huo.
“Kwa sasa tunao jumla ya wagonjwa 17 kati yao Nyamagana na Magu wapo wanane kwa kila wilaya na Ilemela yupo mgonjwa mmoja kwa sasa,” alisema.
Dk Onesmo alisema, hali hiyo inaufanya mkoa huo kuwa na watu waliougua kipindupindu kufikia 926, huku vifo vikiwa 25 tangu uliporitiwa kwa mara ya kwanza katika Wilaya ya Ukerewe, Septemba mwaka huu.
Alisema kwamba jana mtu mmoja alipoteza maisha kutokana na ugonjwa huo wilayani Magu.
Mganga huyo alisema kutokana na idadi ya wagonjwa kuongezeka imewalazimu kuandaa kituo kingine cha kuhudumia wagonjwa katika Wilaya ya Nyamagana.
“Awali, tulikuwa na kituo kimoja cha Igoma, ila kutokana na hali inavyoendelea imetupasa kuwa na kituo kingine katika Kituo cha Afya cha Mkolani baada ya kuona wagonjwa wengi wanatokea maeneo ya Buhongwa ili tuondoe usumbufu wa kuwasafirisha,” alisema Dk Onesmo.
Wakati ugonjwa huo ukiendelea kushika kasi, Jiji la Mwanza limeanza kuzuia uuzwaji wa vyakula vinavyotembezwa mitaani na magengeni, maji ya viroba, matunda yaliyomenywa na pombe za kienyeji.
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Adam Mgoye alisema atakayekaidi agizo hilo watachukua hatua za kisheria.
Hatua hiyo ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu aliyepinga marufuku uuzaji wa matunda holela ili kutokomeza kipindupindu.
Akizungumza hivi karibuni, Mwalimu aliagiza waganga wakuu na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya kuchukua hatua dhidi ya wafanyabiashara wanaouza vyakula bila kuzingatia usalama wa walaji.
Aliwaagiza viongozi hao kuhakikisha matunda hayauzwi sehemu za wazi na maeneo yanayohatarisha usalama wa afya za watu.     

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni