TANGAZO

TANGAZO

Jumanne, 29 Desemba 2015

SASA RASMI, SIMBA YATANGAZA KUANZA KUJENGA UWANJA WAKE WA MAZOEZI

     
Uongozi wa Simba umesema utaanza rasmi kujenga uwanja wao wa mazoezi mwezi ujao.

Rais wa Simba, Evans Aveva amesema watautumia uwanja wao wanaoumiliki kuanza kujenga uwanja wa mazoezi.

“Tutaanza kujenga uwanja kwa ajili ya mazoezi kwa ajili ya kupunguza gharama, kwa siku tunalazimika kulipa hadi laki tatu na nusu kwa mazoezi ya mara moja.
“Kulikuwa kuna mambo ya kupata hati ya umiliki, wakati tunaingia kulikuwa na deni kama la shilingi milioni kumi na mbili hivi,” alisema Aveva.


Uwanja huo ulio katika eneo la Bunju jijini Dar es Salaam, ulinunuliwa na uongozi chini ya Hassan Dalali aliyekuwa mwenyekiti wakati huo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni