TANGAZO

TANGAZO

Jumatano, 30 Desemba 2015

SABABU 5 KWANINI MESUT OZIL NI KIPAJI ADIMU

mesut-ozil-arsenal_3010111.jpg

Tangu atue Arsenal misimu miwili iliyopita kwa ada ya pauni milioni 42 kutoka Real Madrid mchezaji Mesut Özil, klabu yake ya Arsenal imekua hailali njaa.

Wametwaa makombe ya chama cha soka FA cup katika misimu hii miwili mfululizo, Ozil akiwa chachu ya mafanikio hayo. Msimu huu pia Arsenal wako kileleni hadi sasa na tayari Mesut Ozil anakaribia kuvunja rekodi ya kutoa pasi nyingi za magoli (assists) hadi sasa ana assists 16, si kitu cha kawaida.

Kuna kitu lazima ufikirie hivi pamoja na ubahiri wa kiasi hicho wa kocha Arsene Wenger lakini alithubutu kutoa pesa nyingi kiasi hicho pauni milioni 42. Hapa chini nimejaribu kuandika sababu zinazomfanya kijana huyu raia wa Ujerumani kuwa ni kipaji cha kipekee kabisa katika kikosi cha Arsenal na ligi kuu England kwa ujumla;

  1. Umakini (awareness)

Unaweza kuyaangalia macho ya Mesut Ozil ukadhania unavyodhani wewe, lakini kwangu mimi ananikumbusha Ronaldinho Gaucho ama Frank Lampard walivyokua na jicho la kipekee kutazama wapi anaupeleka mpira kabla haujamfika miguuni kwake. Ozil ni aina wachezaji wajanja-wajanja wanapokua uwanjani kitu kinachomfanya awe bora zaidi katika eneo la tatu la kiwanja.

  1. Sio mbinafsi (selflessness)

Huwezi kuwa kinara wa kupiga pasi za mabao kwa wachezaji wenzako kama wewe ni mchoyo. Mesut Ozil kama alivyokua Gaucho ni wachezaji wazuri mno kwa pasi za mwisho na hufikiria zaidi kutoa pasi kuliko kufunga wao. Msimu umefika katikati tayari Ozil amepiga assists 16 ni rekodi ya aina yake.

  1. ‘Touch’ yake ya kwanza

Katika kitu ambacho mshambuliaji Robin Van Persie alikua anafaulu sana anapopata mpira, basi ni ile touch yake ya kwanza ya mpira. Hapa lazima uwe mwanahisabati kwelikweli, vinginevyo huwezi kuwa fundi na utapoteza mipira mingi. Kwa Mesut Ozil touch yake ya kwanza ndio huwa hatari zaidi kwani kutokana na umakini wake anakua tayari alishajua wapi kwa kuupeleka huo mpira.

  1. Mipira iliyokufa (free kick)

Tofauti na ilivyokua wakati Thierry Henry ama Robin Van Persie wakipiga kona ama mipira mingine ya adhabu, Ozil amekua na mipira ya adhabu yenye madhara zaidi kuliko waliomtangulia. Jaribu kuchunguza mipira ya kona ya kijana huyu inapokua inazunguka kutoka katika eneo la kona hadi golini, mara nyingi husababisha hatari zaidi kwa wapinzani.

  1. Mwepesi

Wakati anatua Arsenal ilikua ni ngumu kuona kama angeweza kukidhi misukosuko ya ligi kuu nchini England, ligi ambayo inasifika kwa matumizi makubwa ya nguvu, kasi na pumzi ya kutosha. Lakini sanjari na asili yake ya uvivu (casualness)  katika muonekano wake inamfanya aweze kuwa mwepesi na ‘threat’ katika eneo la tatu la kiwanja kwani ni rahisi pia kuonekana kafanyiwa faulo kutokana na kutokua na ubavu kama walionao akina Mulumbu na Check Tiote.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni