TANGAZO

TANGAZO

Jumanne, 29 Desemba 2015

Rais mpya wa Burkina Faso kuapishwa leo


Aliyekuwa waziri mkuu wa Burkina Faso Roch Mark Christian Kabore, anaapishwa leo kama rais nchi hiyo .
Bwana Kabore ambaye alishinda uchaguzi wa mwezi uliopita, alikuwa mshirika wa karibu wa rais wa zamani Blaise Compaore, ambaye alinyakua mamlaka baada ya mapinduzi ya jeshi, na kutawala taifa hilo kwa miaka 27 hadi mapinduzi ya umma mwaka uliopita.
Kabore alitofautiana na Compaore mwaka uliopita alipotangaza nia ya kuendelea kuongoza.


Viongozi wa mataifa 5 ya Afrika wanatarajiwa kuhudhuria hafla ya kuapishwa kwake.
Tangu ijinyakulie uhuru kutoka kwa Ufransa mwaka wa 1960 Viongozi wengi wa Burkina Faso wamekuwa wakijinyakulia uongozi kwa mtutu wa bunduki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni